# ASANTE MAMA, MOTHER'S DAY CELEBRATION.. ONESHA UPENDO KWA MAMA.
# ASANTE MAMA
Leo ni siku maalum ya Mama, kwa heshima na taadhima nikiongozwa na "unyenyekevu mkubwa" napenda niwapongeze kina mama wote.
Ni magumu mengi mmepitia ili kutusaidia sisi (jamii) kufika hapa tulipo. Mengi mengine yalihatarisha uhai wenu na kuwafanya kupitia ktk kipindi chenye simanzi na majonzi makubwa. Ukiachilia mbali suala la kubeba ujauzito na kuingia "leba". ASANTE MAMA
Unaishi ukiaminishwa mtu ni baba yako kumbe mama kafanya hivyo kwa usalama wake na wako ili uweze kufika sehemu fulani katika maisha. # ASANTE MAMA
Mmekubali kubaki kwenye ndoa "hatarishi" kwa maisha yetu na kuwavumilia kina "baba Fanueli" ili tu kutuinua sisi wanenu. # ASANTE MAMA
Wengi pasipo ridhaa yenu mmeingia kwenye ndoa za mitaala na ukewenza ili watoto wenu tusiteseke maishani. # ASANTE MAMA
Onesha upendo wako kwa mama kwa kutupia comment yako hapo chini,. ukimtaja bi mkubwa wako itapendeza zaidi, asee kama wewe umpendi mama yako basi ukayajenge mapema,,.. # ASANTE MAMA
# Asante Mama
# Love you so much, MAY GOD PROTECTS YOU.
No comments:
Post a Comment