TIOB YAZINDUA RASMI DODOSO LA MAPITIO YA WANACHAMA WAKE +PICHA


Tanzania Institute of Bankers (TIOB) imezindua rasmi mfumo/Dodoso kwa ajiri ya kukusanya maoni na mapendezo ya wanachama juu ya ufanisi wa kozi na mitihani ya taaluma ya kibenki zinazotolewa pamoja na maoni ya watanzania kwa ujumla watakaopenda kujua zaidi kuhusu TIOB kupitia barua pepe na tovuti ya taasisi.

TIOB ni taasisi inayosimamia taaluma ya sekta ya kibenki Tanzania ambayo inashirikiana na mabenki yote yaliyopewa leseni na benki kuu, inafanya usiamamizi huu kwa kutoa vyeti vya taaluma kwa wanachama pamoja na kutunza taarifa zao.

Leo tunatangaza rasmi kwanzia tarehe 31 Jully 2017 mpaka 30 September 2017 tutakua tunapokea maoni ya wanachama na watanzania wote mabao wangependa kujua juu ya kozi na huduma nyingine zinazotolewa na TIOB kupitia tovuti ya taasisi ambayo ni www.tiob.or.tz  


Aidha, TIOB imetangaza matokeo ya mwezi May 2017, Ndugu Saad Banzi – Msajili wa TIOB  ameyatangaza matokeo hayo ya watahiniwa katika mithani ya Nyanja ya kibenki, ambapo kulikua na watahiniwa 800 walijisajili kwa ajili ya mitihani, katika hao watahiniwa 115 waliweza kufaulu mitihani yao katika Nyanja za Certificate of Banking (9), Certified Proffesional Bnkers ( 97) na Specialist Programs (9).

Idadi hii ya watahiniwa 800 waliojisajili ni kati ya wafanyakazi wa sekta ya benki 15,000 walioko nchini, vile vile taasisi imeanza kupokea maombi kwa wale wanaohitaji kufanya mitihani hiyo kwa mwezi wa November, wanaweza kufika ofisi za taasisi zilizoko Mirambo Street/Samora NIC House 10th floor.
Mkurugenzi wa mafunzo ameongeza kwa kutaja kozi za muda mfupi zinazotolewa na taasisi ambapo kwa mwezi wa nane, kutakua na kozi za :

Ø  Assets and liability Management ( 9 – 11 Aug 2017 )

Ø  Bank Branch Management ( 15 – 18 Aug 2017)

Ø  Sales and Customer Care ( 22 – 25 Aug 2017 )



“TIOB imejipanga kuendana na uvumbuzi ambao umefika hapa nchini, wa aina ya huduma za kibenki na ule wa kidigitali katika hutoaji wa huduma za sekta hii ya kibenki ambao kwa kiasi kukibwa umesaaidia nchi kukua, taasisi hii inatoa elimu na kuwaanda wahitimu wake kwa kufuata misingi ya sharia ya utoaji huduma katika sekta ya kibenki,” – Patrick Mususa Mkurugenzi Mtendaji wa TIOB

Kwa taarifa hizi, Taasisi inaomba ushirikiano katika kujaza na kujibu maswali mbalimbali yaliyopo kwenye dodoso hilo, kwa usahihi na ukweli kwaajili ya kufanikisha mapitio haya.
Kwa Taarifa Zaidi wasiliana  na:

The Executive Director
Tanzania Institute of Bankers
P. o. Box 8182, Dar es Salaam.
Telephone: 22 2112605

No comments:

This Website Is Developed & Maintained By Jesse. Powered by Blogger.