IBRAHIMOVIC KUONDOKA PSG, ANAKWENDA TIMU GANI?

340E2B9F00000578-3588474-image-a-1_1463128830831


Mshambuliaji wa klabu ya Paris St-Germain Zlatan Ibrahimovic anaondoka katika klabu hiyo mwishoni mwa msimu huu.

Mkataba wa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 34 unakamilika msimu huu na amehusishwa na uhamisho wa Manchester United,kilabu ya Los Angels Galaxy na AC Milan.
”Ninafurahia”,alisema.”Niliwasili kama mfalme na sasa naondoka kama kigogo lakini ntarudi”.
PSG imesema kuwa Ibrahimovic anaondoka kama mshambuliaji bora na mchezaji bora zaidi katika historia ya kilabu hiyo.
Ibrahimovic ameifungia mabao mengi zaidi klabu hiyo licha ya kujiunga nayo mwaka 2012 aiwa amefunga mabao 152 katika mechi 178.
PSG imeshinda taji la Ligue 1 kila msimu tangu Ibrahimovic ajiunge na kilabu hiyo.

No comments:

This Website Is Developed & Maintained By Jesse. Powered by Blogger.