Mwenyekiti wa NCCR Mageuzi Injinia
James Fransis Mbatia amesema kwamba maamuzi yoyote ambayo kambi ya
upinzani itayafanya endapo wataitwa na kamati ya maridhiano juu ya
kususia Bunge wao watakachoangalia ni maslahi ya kitaifa.
Injinia Mbatia ameyasema hayo Jijini
Dar es salaam kuhusu hoja ya wao kukutanishwa na kamati ya maridhiano
kujadili kitendo chao cha kususia bunge la bajeti.
”Sisi
kabla ya kufanya jambo lolote tunaangalia mama Tanzania kwanza, swala
la maridhiano limekuwa jambo letu mara zote , tangu tumeanza masuala ya
katiba pamoja na mambo ya demokrasia tuna” amesema Mbatia.
”Sisi hatujadili mtu tunajadili mfumo,
Bunge kwa mujibu wa katiba linatakiwa lisimamie serikali na kuishauri
kwa kuheshimu utu na kuhakikisha yale tunayoyafanya yanakuwa na maslahi
ya taifa”- Amesema Mbatia.
Mgogoro wetu na Naibu Spika ni kwamba
anaongoza Bunge kwa kuagizwa na serikali na hii itaonekana wazi kwamba
hoja ya maslahi ya wabunge wabunge wa CCM waliosema hapana walikuwa ni
wengi na walikuwa wao kwa wao lakini akasema anatumia kura ya veto hivyo
hoja hiyo imepita.
Mbatia amehitimisha kwa kusema
watanzania wategemee kama hali ya maridhiano haitapatikana wategemee
mambo hayohayo ya kususia mambo kurudi kwenye jamii mfano tuu suala la
VAT serikali imeshindwa kulifafanua kwa kuwa waziri amesema la kwake
gavana wa benki akasema la kwake na mkurugenzi wa tra akasema la kwake.
TUTASUSUIA KILA KITU.... MH. MBATIA
Reviewed by JANASIOLEO
on
11:39:00 PM
Rating: 5
No comments:
Post a Comment