PAPA FRANCIS AMEMTAWAZA LEO MAMA TERESA KUWA " MTAKATIFU "

Mama Tereza atawazwa kuwa mtakatifu

Maelfu ya watu wameshuhudia ibada ya kutawazwa kuwa mtakatifu, ambapo Papa Francis amemtangaza mtawa Mama Teresa kuwa mtakatifu.
Raia huyo wa Albania ambaye alifariki mwaka wa 1997 alianzisha shirika la hisani la kimishenari ili kuwasaidia walala hoi katika mtaa wa mabanda wa Calcutta nchini India.
Atajulikana kuwa mtakatifu Teresa wa Calcutta.
Waandishi wanasema kuwa maisha yake yanaenda sambamba na maono ya Papa Francis kuhusu kanisa linalojikakamua kuwasaidai watu masikini.
Lakini wakosoaji wanasema kuwa Mama Teresa hakuwasaidia watu waliokuwa wagonjwa ,na alilaumiwa kwa kujaribu kuwabadilisha dini watu masikini wa kabila la Hindu nchini India kuwa Wakristo.

No comments:

This Website Is Developed & Maintained By Jesse. Powered by Blogger.