RAIS JOHN POMBE MAGUFULI ATAKA WIZARA NA TAASISI ZA SERIKALI KULIPA KODI

Rais John Magufuli akizungumza na waliokuwa wakazi wa Magomeni Kota alipokutana nao jana, Dar es Salaam. (Picha na Fadhili Akida).

Akizungumza na wazee waliokuwa wakazi wa eneo la Magomeni Kota jijini Dar es Salaam jana, Rais Magufuli alisema tayari ameshatoa maagizo kwa taasisi zozote za serikali ikiwemo wizara zinazodaiwa na NHC, kuhakikisha zinakamilisha kulipa madeni yao ndani ya siku saba.

“Wasipolipa nakuagiza bwana Mchechu watolee nje mali zao kama ulivyomtolea nje yule jamaa. Usiogope mtoe mtu yeyote asiyelipa pango hata kama ni serikali, waziri, Ukawa, Rais au CCM. Lazima watu hawa wakulipe ili upate fedha za kuliendesha shirika hili,” alisisitiza Rais Magufuli

Rais John Magufuli ametoa siku saba kwa taasisi zote za serikali zinazodaiwa malimbikizo ya kodi na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), kuhakikisha zinalipa madeni yao, vinginevyo mali zao zitatolewa nje.

Dk Magufuli amemtaka Mkurugenzi Mkuu wa shirika hilo, Nehemia Mchechu kutomuogopa mtu yeyote awe Rais, Waziri, CCM, Chadema au kiongozi yeyote wa serikali endapo hajalipa pango lake la nyumba, atolewe nje mali zake.

No comments:

This Website Is Developed & Maintained By Jesse. Powered by Blogger.