BEN POL : KWANZIA 2017 NITATOZA MILLION 10 KWA KOLABO



Ben Pol amesema kuanzia mwakani atakuwa akitoa dola 5,000 kwa kila kolabo ambayo ni zaidi ya shilingi milioni 10 za Kitanzania.
“Kuelekea 2017 bei yangu ya Collabo itakuwa $5000. So kama una project na mimi tuwasiliane before 31st Dec 2016,” aliandika Ben kwenye Twitter.
“Ni kweli, ila kama wimbo ni mkali tunaweza kukaa mezani na huyo mtu akanipa sehemu ya umiliki wa hiyo kazi,” Ben ameongeza baada ya kuulizwa kama amedhamiria kweli.
“Kwanza nataka kupunguza idadi ya colabo ili nifanye chache za walio serious na wanaoweza kupush hizo project. Mfano mtu hawezi kukulipa dola elfu 5 halafu akaiweka ngoma kwenye album, au akaiweka ndani tu,” amesisitiza.
“Pia itasaidia kwangu kufikiria zaidi kwenye hiyo kazi, hakuna mtu atakulipa dola 5 halafu akatarajia disappointment, so ita-benefit kwa pande zote.”

No comments:

This Website Is Developed & Maintained By Jesse. Powered by Blogger.