HII HAIJAWI TOKEA:- MAREHEMU ATEULIWA KUSIMAMIA MECHI NIGERIA.




Mwanamume aliyefariki ameteuliwa kusimamia mechi ya soka nchini Nigeria ambayo itachezwa Jumapili.
Wale Akinsanya (jina la referee) aliteuliwa kuwa mwamuzi kwenye mechi baina ya Warri Wolves na Giwa FC katika mji wa Warri kusini mwa Nigeria, gazeti la Punch la Nigeria limeripoti.
Hii ni licha ya kwamba Akinsanya alifariki tarehe 22 Januari 2016 wakati wa kufanywa kwa mtihani wa Fifa Cooper Test, ambao hutumiwa kuamua iwapo marefarii wanatosha kuendelea kusimamia mechi.
Aliteuliwa kusimamia mechi hiyo na mrengo wa Shirikisho la Soka la Nigeria (NFF) unaoongozwa na Chris Giwa.
shirika la soka la Nigeria, NFF  bado alijatamka kitu kuhusu hili swala..

No comments:

This Website Is Developed & Maintained By Jesse. Powered by Blogger.