RAIS WA ZAMANI WA BURUNDI AFARIKI DUNIA


4  May 2016

Rais wa zamani wa Burundi Kanali Jean-Baptiste Bagaza amefariki akitibiwa nchini Ubelgiji.
Kanali Bagaza amekuwa akitibiwa kwa muda katika hospitali ya Sainte Elisabeth mjini Brussels.
"Imethibitishwa, rais wa zamani Jean Baptiste Bagaza amefariki dunia akiwa nchini Ubelgiji,2 ameandika mshauri wa rais wa Burundi Willy Nyamitwe kwenye Twitter.
"Alikuwa seneta maisha.”
Kanali Bagaza aliingia madarakani Novemba 1976 kupitia mapinduzi ya kijeshi.
Aliondolewa madarakani kupitia mapinduzi mengine yaliyoongozwa na binamu wake Meja Pierre Buyoya Septemba 1987.

No comments:

This Website Is Developed & Maintained By Jesse. Powered by Blogger.