WAFUASI WA PROF.LIPUMBA WAKUSANYIKA KWENYE OFISI ZA CUF KUMPOKEA MWENYEKITI WAO NA KUMUINGIZA OFISINI



Vikundi vya wafuasi wa Profesa Ibrahim Lipumba wamekusanyika katika Ofisi za CUF Buguruni wakisubiri kumpokea mwenyekiti huyo wa zamani na kumwingiza ofisini.

Wanachama hao wanadai wana barua ya Msajili wa vyama vya siasa inayomtambua Profesa Lipumba kama mwenyekiti halali wa CUF.

Geti la ofisi za CUF limefungwa na ndani hakuna kiongozi yeyote wa chama.

Mashabiki hao wa Lipumba wanaoimba na kucheza, wanasema msafara wa Profesa uko njiani kuelekea kwenye ofisi hizo za makao makuu ya chama hicho.

Alipoulizwa kuhusu hali hiyo, Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi ya CUF, Julius Mtatiro amesema ndio wamepokea barua ya msajili na bado wanaisoma ili kuona imeelekeza kitu gani.

Hata hivyo, Mtatiro amesema kwa vyovyote vile msajili wa vyama vya siasa hana mamlaka ya kuingilia maamuzi ya vikao vya chama chochote cha siasa.

No comments:

This Website Is Developed & Maintained By Jesse. Powered by Blogger.