GODBLESS LEMA ANYIMWA DHAMANA KWA MARA NYINGINE



Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema amekwaa kisiki kwa mara nyingine katika harakati za kuomba dhamana baada ya Mahakama Kuu Kanda ya Arusha kutupilia mbali ombi la marejeo ya kesi yake na kushauri kuwa Mawakili wake wakate rufaa ya kupinga zuio la dhamana

Mawakili wa Lema leo walikuwa wakirusha karata hiyo kwa mara ya tatu baada ya mara mbili za awali mteja wao kushindwa kupata dhamana.

Lema amesota rumande tangu alipokamatwa Novemba 3, 2016 akiwa mkoani Dodoma na kusafirishwa hadi Arusha ambapo anashtakiwa kwa kosa la uchochezi dhidi ya Rais Dkt Magufuli.

No comments:

This Website Is Developed & Maintained By Jesse. Powered by Blogger.