HUENDA BASATA WAKAIFUNGIA VIDEO YA RICH MAVOKO FT DIAMOND YA KOKORO
Baraza la Sanaa la Taifa, BASATA limehisi kuna udhalilishwaji wa wanawake kwenye video hiyo na limesema litatoa tamko lake iwapo litaifungia video hiyo au lah!
“Ktk kusimamia maadili ktk Sanaa & udhalilishaji wanawake tuko thabiti.Video ya #kokoro ya #Mavoko inapitia uhakiki.Taarifa itatoka,” limeandika baraza hilo kwenye akaunti yake ya Twitter.
Video ya wimbo huo iliyofanyika nchini Afrika Kusini inaonesha wanawake waliopo kwenye Jacuzzi huku maziwa yao yakiwa wazi licha ya kupakwa rangi ya dhahabu.
Ktk kusimamia maadili ktk Sanaa & udhalilishaji wanawake tuko https://t.co/OZK6NKbutn ya #kokoro ya #Mavoko inapitia uhakiki.Taarifa itatoka— Baraza la Sanaa (@BasataTanzania) November 23, 2016
No comments:
Post a Comment