DIAMOND PLATNUMZ AVUNJA RECORD .... read more

TM UPDATES: 
 
          DIAMOND DANGOTE AVUNJA RECORD KWA KUONGOZA KUWA NA MAFANS WENGI KATIKA INSTAGRAM KWA WASANII WA AFRICA NA KUMPITA MSANII MKUBWA WA MAREKANI NEYO.... 





Msanii wa muziki wa kizazi kipya nchini Tanzania anayejulikana kama Diamond platnumz anayefanya vizuri katika industry ya muziki wa kizazi kipya akiwa chini ya lebal ya WCB, na manajer Tale ameweka rikopi kali zaidi kwa wasanii wakubwa wa Africa kwa kuwaongoza wasanii hao kwa kuwa na jumla ya followers wengi katika mtandao wa instagram wakiwa ni follower million mbili (2mill).

 Diamond platnumz anayewika kwa wimbo wa sasa alioimba na msanii aliyeko chini yake harmonizer unaokwenda kwa jina la BADO, kadri siku zinaposogea diamond platnumz amekuwa akifanya vizuri ndani na nje ya kimataifa uku akikaririwa kusema ataendelea na moto huo huo.

Katika mitandao ya kijamii mashabiki wanao mfatilia wamezidi kuongezeka katika facebook, twitter na zaidi katika mtandao wa instagram na pia katika mtandao wa youtube diamond platnumz nyimbo zake zimekua zikitazmwa na watu wengi ndani na nje ya nchi haswa pale anapotoa nyimbo mpya.















Diamond ambaye sasa yuko na bibie anayekwenda kwa jina la Zari the boss lady, akiwa pia ni mama wa mtoto wake wa kike anayeitwa Tiffa .. kuzaliwa kwa mtoto huyu wa diamond kumemuongezea followers wengi katika mitandao ya kijamii kwa kile amabacho kilikua kinasemekana kuwa Tiffa sio mtoto wa diamond.

Pia, kufanya kwake vizuri katika tasnia ya music anaoufanya na kujiongeza kwake kwa kufanya collabo na wasanii wakubwa kama vile Davido, KO, Mafikizolo, Mr. flavor, Kcee, Iyanya na wengine wengi ikiwemo P square ambayo bado haijatoka kunamuongezea mashabiki nje na ndani nchi.

Msanii huyu kutokana na takwimu za hivi karibuni amekuwa akiongoza kwa kuwa na follower wengi katika instagram wakiwa ni 2M ambapo amewapita wasanii wote wakubwa wa Afrika akiwemo Davido ambaye ana followers 1.9M na Wizkid akiwa na follower  1.6M


Diamond platnumz amempita pia msanii mkubwa wa marekani anayekwenda kwa jina la Neyo ambapo Neyo anajumla ya followers 1.7M wakati Diamond akimpita kwa followers laki tatu ( 300,000).

 Ikumbukwe kwamba,  diamond amekua akikaririwa akisema kwamba atafanya collabo na msanii uyo mkubwa wa marekan Neyo, na amekua akipost picture wakiwa studio na msanii uyo kama harakati za kurecord nyimbo na msanii huyo mkubwa wa marekani.




Tuendelee kusubiri makubwa kutoka kwa msanii huyu kipenzi cha wengii ambaye amekua akipeperusha bendera ya Tanzania vizuri nje ya nchi kwani hadi sasa Diamond platnumz amepata tuzo zaidi ya 15 zikiwemo zile za MTVmama awards, Channel O awards, Best live Acts  na tuzo nyingine nyingi..


















 

No comments:

This Website Is Developed & Maintained By Jesse. Powered by Blogger.