DUBAI: WANASWA WAKIENDESHA MAGARI KILOMITA 300 KWA SAA
Polisi wanasa magari magari 81 wakiwa wanaendesha kilomita 300 kwa saa. |
Idara ya polisi katika milki za kiarabu huko Dubai imekamata magari 81 ambayo yalikuwa yakiendeshwa kasi ya zaidi ya kilomita 300 kwa saa.
Hatua hii inafuatia uchunguzi katika barabara za kutoka nje ya mji ambapo wenye magari waling'oa namba za usajili wa magari hayo kisha wakashindana.
Polisi wanashuku kuwa mashindano hayo yanayokiuka sheria za barabarani mbali na kuhatarisha maisha ya waendeshaji wengine wa magari huwa yanaandaliwa na matajiri wanaomiliki magari ya kifahari.
Polisi walilazimika kutumia magari ya kifahari kuwanasa madereva hao watundu |
Aid polisi wanashuku matajiri hao huweka dau kisha kuwaajiri madereva kushindana mabarabarani.
Polisi walikuwa na wakati mgumu kuwakamata washukiwa kwani waliendesha magari yao kwa kasi zaidi ya kilomita 290 kwa saa.
Polisi walimudu tu kuwatia mbaroni baada yao pia kuyatumia magari ya kifahari yanayomilikiwa na polisi.
No comments:
Post a Comment