FRIDAY XO : WIVU NI KITU CHA MUHIMU KATIKA MAPENZI LAKINI UKIZIDI UNAKERA NA NI SUMU



Wivu katika mapenzi unamaanisha mtu kumiliki mpenzi wake peke yake pasipo kuingiliwa na mwingine, kwa maana nyingine kuonyesha unampenda na kumjali ila ukizidi unakuwa sumu.

Lakini kwa kiumbe kinachovuta pumzi lazima kiwe katika hali hiyo na kama bado unavuta pumzi basi hujui nini maana ya kupenda. Lakini kwa yeyote anayeijua thamani ya kupenda lazima atakuwa anajua maana ya wivu.

Wivu katika mapenzi ndiyo chachandu kwa mtu kujua kweli anapendwa. Huwezi kuwa na mke au mume akichelewa au kusimama mazingira yasiyo eleweka ukae kimya, ujue lazima kuna walakini akilini mwako.

Lakini wivu uliovuka mipaka ambao huwa kero kwa wengine. Wapo wanaume au wanawake huwaonea wivu hata dada au kaka yako hiyo ni kero sio Mapenzi.

No comments:

This Website Is Developed & Maintained By Jesse. Powered by Blogger.