BARCELONA YAWEKA HISTORIA MPYA KWENYE SOKA..TAZAMA REKODI HIZI WALIZOVUNJA

Image result for barcelona vs psg

Sergi Roberto alifunga bao la 6 kwa mkwaju wa mwisho wa mchezo, na hivyo kufanya matokeo ya jumla kuwa 6-5 kwenye mchezo uliopigwa kwenye dimba la Nou Camp.
Barcelona walifunga magoli matatu katika dakika saba za mwisho. Walikuwa wakiongoza kwa 3-1.
Wiki tatu zilizopita PSG iliifunga Barcelona magoli 4-0 mjini Paris.
Hatua ya kurejesha magoli yote hayo ni kubwa kuwahi kushuhudiwa katika historia ya UEFA, na sasa Barcelona wana kila nafasi ya kunyanyua kombe la Klabu Bingwa Ulaya kwa mara ya pili katika kipindi cha miaka mitatu.
Image result for barcelona vs psg
Katika mchezo mwingine, Pierre Emerick Aubameyang alipachika 'hat trick' na kuipeleka Borussia Dortmund katika robo fainali dhidi ya Benfica
Na hizi ndizo rekodi kubwa walizovunja barcelona jana ... 
  • Borussia Monchengladbach v Real Madrid (1985-86 Uefa Cup)
Real waliikaribisha Borussia Monchengladbach kwenye mchezo wa marudiano katika raundi tatu ya Uefa Cup baada ya miamba hiyo ya Ujerumani kushinda 5-1 kwenye mchezo wao wa nyumbani lakini Madrid wakaweza kutengua matokeo kwa kupata ushindi wa magoli 4-0 na kufuzu hatua ya nane bora.
  • Leixoes v La Chaux-de-Fonds (1961-61 Cup Winners’ Cup)
Leixoes walikuwa wamechapwa 6-2 huko La Chaux-de-Fonds, lakini mabingwa hao wa zamani wa Uswis walishinda 5-0 kwenye uwanja wao wa Estádio do Mar na kusonga mbele kwenye mashindano.
  • Partizan v QPR (1984-85 Uefa Cup)
QPR ilishinda 6-2 kwenye mechi ya kwanza iliyochezwa kwenye uwanja wa Highbury kwa sababu uwanja wao wa Loftus Road ulikuwa wa nyasi za plastic, lakini wakapoteza game ya pili kwa kipigo cha magoli 4-0 kwenye uwanja wa Belgrade na kutupwa nje ya mashindano kwa sheria ya goli la ugenini.

No comments:

This Website Is Developed & Maintained By Jesse. Powered by Blogger.