MWAKYEMBE ACHACHAMA SERENGETI BOYS KUZUIWA BARABARANI, ASEMA HAYA



Waziri mwenye dhamana ya michezo Dr. Harrison Mwakyembe amekuja juu baada ya kusikia kwamba timu ya taifa ya vijana chini ya miaka 17 ‘Serengeti Boys’ ilishushwa kwenye mabasi na TRA wakati ipo njiani kwenda kwa makamu wa Rais mama Samia Suluhu Hassani ambaye aliialika timu hiyo kwa ajili ya kupata nao chakula cha jioni.
Mwakyembe amesema ni aibu kwa taifa wakati kipindi hiki kukiwa na kampeni za kuhamasisha watanzania na wachezaji ili timu ifanye vizuri halafu wanakuja watu wengine wanarudisha nyuma jitihada zinazofanywa.
“Vijana wetu walikuwa wanakuja kwako basi lao likasimamishwa na watu wa TRA wakaondolewa kwenye mabasi magari yakachukuliwa, ikabidi viongozi wa TFF waanze kutafuta magari mengine, sijui wameingia kwenye daladala ndiyo wamewaleta hapa.”
“Nataka niseme kitu kimoja kama kiongozi wa hii Wizara, suala la kodi ni suala muhimu na ni lazima kila mtu alipe, hilo halina mbadala wala msamaha, lakini natumia fursa hii kuwasisitiza TRA kutumia busara katika kukusanya kodi.”
“Baada ya kupata hizi taarifa, namwagiza katibu wangu mkuu kukaa na katibu mkuu wa Wizara ya Fedha na viongozi wa TRA wakae pamoja, haya mambo yanatia aibu. Tunakwenda kwa kiongozi wetu wan chi, wewe ndio unaona hiyo fursa kwako, nani atakupa mabilioni hayo ya fedha kwa kusimamisha magari barabarani?”

No comments:

This Website Is Developed & Maintained By Jesse. Powered by Blogger.