CUF YA MAALIM SEIF KULIAMSHA " DUDE " KUJIBU YA LIPUMBA KUFUKUZA WABUNGE 8

Image result for maalim seif cuf


Naibu Katibu wa CUF- Zanzibar, Nassor Ahmed Mazrui alisema wamepata taarifa za uamuzi wa baraza kuu hilo na kwamba wataitisha la kwao ili kujibu mapigo.

Mazrui alisema kabla ya kuitisha Baraza Kuu la Uongozi la Taifa, kikao cha kamati ya Utendaji kitakutana kwa ajili ya kujadili suala hilo kwa kina na kuwataka wanachama wa CUF kuwa wavumilivu.

“Tutaitisha Baraza Kuu la Uongozi la Taifa halali kujadili haya yaliyofanywa na upande Profesa Lipumba. Hapa ninavyoongea na wewe ninaongoza kikao cha maandalizi kuhusiana na kamati ya utendaji na baraza kuu.

“Baraza Kuu la Uongozi la Taifa halali, litatoa uamuzi nini way forwad (mwelekeo) wa uamuzi uliofanywa na hawa watu ambao wengine tuliwasimamisha uanachama,” alisema Mazrui ambaye ni mmoja kati ya viongozi watakaoitwa kwa ajili ya mahojiano kwa tuhumu za kukihujumu chama hicho kwa mujibu wa Profesa Lipumba.

Akizungumzia mgogoro huo mpya, Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi alisema utatolewa maelezo mara baada ya kujadiliwa na ofisi yake.

Kuhusu hatua hiyo, mmoja wa wabunge waliofukuzwa uanachama, Khadija Salum alisema anasubiri maelekezo kutoka kwa kiongozi wa chama chake, Maalim Seif ambaye ni katibu mkuu wa CUF kwa sababu katiba haimtambui Profesa Lipumba.

“Inakuwaje mtu ambaye hata si mwanachama anajitokeza na kukufuta uanachama? Haikubaliki, mimi nitaendelea kufanya wajibu wangu,” alisema.

Mbunge mwingine, Salma Mohamed alisema hautambui uongozi wa Profesa Lipumba.

“Si halali kwa kundi la watu au mtu mmoja kutoa maamuzi wakati kesi ipo mahakamani,” alisema.

No comments:

This Website Is Developed & Maintained By Jesse. Powered by Blogger.